Hamasa za Maisha


Hizi ni Nukuu (Quotes) zinazoweza kukuhamasisha Katika kufikia ndoto zako, Binafsi hunipa Ari na Moyo wa Kufanya kazi kwa bidii ili kuyatimiza malengo yangu, natumaini  na wewe zinaweza kuwa Kichocheo Kikubwa cha mafanikio kwako pia.

1.Muujiza uliopo kwenye
   kufanikiwa ni kuacha
   kutamani na kuanza
   kutenda. By J. Kweka

2.Usikubali uoga wako
   uamue hatima ya maisha
   yako.

3.Anguka mara NANE
   lakini simama mara
   ya TISA. 
   Chinese Proveb.

4.Ujasiri siyo Kutokuwepo
   kwa HOFU, bali ni
   kufanya  kitu ingawa
   kuna HOFU.

5.Ukitaka kushindwa
   kufika unakokwenda ni
   kujaribu kumtupia jiwe
   kila mbwa anaye
   kubwekea njiani.By
   Winston Churchhill.

6.Furaha ya Maisha siyo
   kuwa na pesa nyingi, bali
   ni kuona pesa yako
   inasaidia wale
   wasiyojiweza.

7.Usipende kufanya
  mambo makubwa sana,
  Bali fanya yale
  madogomadogo kwa
  ufanisi mkubwa. By
  St. Theresa of Calcutta.

8.Huwezi Kufanikiwa
   mpaka upende kazi ile
   unayoifanya.    
   By Dale  Carnegie.

9.Ukitaka kufanya
   mabadiliko makubwa
   katika maisha, acha
   kuangalia ukubwa wa
   tatizo lako. 
   By T. Harv Eker.

10.Watu wengi hawaishi
     ndoto zao, kwa kuwa
     wanaishi uoga wao. 
     By Les Brown

11.Usiache yale usiyoweza
     kufanya yaingilie na
     yale unayoweza
     kufanya.

12.Ni bora kufeli katika
     uhalisia kuliko kufaulu
     katika kuiga. By Herman
     Melville.

13.Vitu vingi vya maana
      katika Dunia vilifanywa
     na watu ambao walizidi
     kujaribu hata pale
     mambo yalivyoonekana
     yameshindikana kabisa.
     Dale Carnegie.

14.Haijawahi kuchorwa
     mahali popote picha ya
     kuvutia ya mtu mvivu.
     By Oprah Winfrey.

15.Mafanikio yako
     hupimwa kwa ukubwa
     wa vikwazo ulivyopitia
     Kufikia Malengo
     yako. By  J.  Kweka.

16.Inakupasa kuamka kila
     asubuhi na hamasa,
     kama unataka kulala
     usiku ukiwa
     umeridhika. By George
     Lorimer.

17.Hamasa ndiyo
     inayokufanya uanze
     safari yako ya
     mafanikio. Tabia ndiyo
     inayokufanya uendelee
     mbele katika mafanikio.
     By Jim Ryun.

18.Uoga wetu katika
     maisha usiwe katika
     kushindwa,  bali katika
     kushinda vitu visivyo na
     maana. By Francis Chan

19.Akili ndogo hushikwa
     na kutishwa na hali
     ngumu,  Wakati Akili
     kubwa huvuka na
     kupanda
     juu ya matatizo.

20.Inaweza ikakubidi
     kupigana katika vita
     zaidi ya mara moja ili
     ushinde.

21.Mafanikio siyo
     kutokufanya makosa,
     Bali ni kuhakikisha
     hurudii kosa ulilolifanya
     zaidi ya mara moja. By
     George Bernard Shaw.

22.Uwekezaji mzuri ni ule
     wa kuwekeza katika
     Maarifa,  kwani
     matunda yake
     utayafaidi daima. 
     By Warren Buffett.

23.Kama unaweza
     kuhesabu hela zako,
     Basi inakubidi ufanye
     kazi kwa bidii sana. 
     By Genius Ginimbi.

24.Kuzaliwa masikini si
     kosa lako,  Bali kufa
     masikini ni kosa lako. 
     By BillGate.

25.Kupata 0 katika
     mtihani haimaanishi
     huwezi, ni kwamba una
     njia nyingine 100 za
     kufanya vizuri zaidi. 
     By J. Kweka.

26.Muda mzuri wa
     kupanda mti ni miaka
     10 iliyopita, lakini muda
     mwingine mzuri zaidi ni
     sasa. Chinese Proverb

27.Kitu pekee
     kinachokutenganisha
     wewe na mafanikio
     yako ni Fikra na
     mtazamo wako.

28.Kuwa hodari kusimamia
     kile unachoamini hata
     kama ukiishia
     kusimama mwenyewe.

29.Ni bora kujaribu na
     kushindwa,  kuliko
     kutojaribu kabisa,
     By Roy T Bennet.

30.Mtu pekee ambaye
     hajawahi kukosea ni 
     yule ambaye hakuwahi 
     kujaribu  kitu kipya.


31.Kuna Wakati utafika
     utagundua muda wa
     kufanya yale Mambo
     Uyapendayo ulishapita,
     Lakini wakati mwingine
     mzuri ni sasa.

32.Hujachelewa kuwa yule
      unayetamani kuwa.

33.Kula chakula kama
     dawa kwa ajili yako;
     Vinginevyo utakuja 
    kula dawa kama chakula
     chako. By Michael Osae

34.Mafanikio ni jumla ya
     nguvu kazi ndogondogo
     zinazorudiwa kila siku.
     By Robert Collier.

35.Mwanzo wa Kila
     Mafanikio ni njaa na kiu
     ya hayo mafanikio. 
     By J. Kweka.

36.Usisubiri fursa itokee,
     Bali Tengeneza fursa
     yako mwenyewe. 
     By Chris Grosser.

37.Wajasiriamali wenye
     mafanikio ni watoaji na
     si wachukuaji.

38.Vitu vizuri huja kwa
      mtu yule anayevisubiri,
      Lakini Mafanikio huja
      kwa mtu mwenye
     kutoka nje na kuyafuata.

39.Kama uko tayari
     kufanya kazi kwa nguvu
     zaidi ya unavyolipwa,
     Mwishowe utalipwa
     zaidi ya kazi
     unayofanya. 
     By J. Kweka.

40.Mafanikio ni
     kinachokuja baada ya
     kuacha kujipa 
     vijisababu.
     By Luis Galarza.

41.Akili yako ina nguvu
      kuliko unavyodhani,  
      Jaza akili yako na
      maneno na fikra
      chanya na utaona
      Mafanikio yake.

42.Ili Ufanikiwe, inakubidi
     Ujaribu kufanya kitu
     kimoja kila siku
     kinachokutisha.

43.Mafanikio 
    yameungwa na
    mipango.     
    Na ukishindwa kupanga,
    Umepanga kushindwa.
    By John Beckley.

44.Ukitaka kuwa wa
     thamani, tengeneza
     thamani kwa wengine
     Kwanza. By J. Kweka.

45.Jifunze Elimu zote,
     Lakini Elimu ya fedha
     ina Umuhimu Wake. 
     By J. Kweka.

46.Katika Maisha Kuna
     siku mbili tu muhimu,
     nazo ni Siku ya
     kuzaliwa na ya pili 
     ni Siku ya Kujua 
     kwanini Ulizaliwa. 
     By J. Kweka.

47.Ukitaka kuwa mtu wa
     mafanikio, Kuwa makini
     sana na kitu Ulacho,
     Usomacho, Uangaliacho
     na Marafiki
     wanaokuzunguka. 
     By J. Kweka.

48.Ukitaka kumla tembo
     usiangalie ukubwa
     wake, Na ukitaka 
     kufanikisha jambo
     Anza kidogokidogo.

49.Vita vya kwanza
    vinavyomtesa binadamu
     ni hofu, na vya pili ni
     kukata tamaa. 
     By J. Kweka

50.Wengi tunatamani
     kusikia kisemwacho,
     lakini hatuna mbinu za
     kusikiliza. By J. Kweka.


51.Usikimbilie Pesa, bali
     penda kile
     unachokifanya na
     kifanye kwa ufanisi
     mkubwa nayo pesa
     itakukimbilia.
     By Samantha Wills.

52.Kufanikiwa ni kama
    fumbo, Ukiona Maisha
    yanakupa Limao; Wewe
    tumia hizo limao
    kutengenezea juisi.
    By J. Kweka.

53.Ukipewa masaa 
     Matano kukata mti, 
     Tumia masaa matatu
     kunolea Shoka.
     By Abraham Lincoln.
    
54.Linda sana mdomo
    wako, Ukiufungua ujue
    Unaiambia dunia kuwa
    wewe ni mtu wa aina
    gani.
    By Les Brown.

55.Tunapata afya kwa kula
     vyakula, na tunapata
     maarifa kwa kusoma
     vitabu. By J. Kweka.

56.Ili kufanikiwa, katika
     kamusi yako futa neno
     "Haiwezekani" 
     By Napoleon Hill.

57.Fursa ni kama embe,
     wakati unasubiri liive,
     wengine wanalila kwa
     chumvi. By J. Kweka.

58.Ukiacha kusoma Vitabu,
      ujue usha anza kufa
      taratibu. By J. Kweka.

59.Usipojiajiri kwenye
     kutimiza ndoto zako,
     Basi utaajiriwa kutimiza
     za mwenzako.

60.Kuwa wa kwanza
     kujaribu na kushindwa, 
     ili upate muda mzuri wa
     kujifunza. By J. Kweka.

61.Kiongozi Bora ni 
     msomaji mzuri wa 
     Vitabu.

62.Silaha nzuri ya
    kutokukosolewa ni hii,
    Usijaribu chochote,
    Usianzishe chochote, na
    Usifanye chochote.
    By J. Kweka.

63.Katika kukamilisha
  safari yako ya mafanikio,  
  Jifunze kukaa kimya. 
  By J. Kweka.

64.Ubunifu ndiyo ajira
     pekee ya Kudumu,
     Kwa hiyo heshimu
     ubunifu wako.
     By J. Kweka

65.Siri ya Mafanikio yetu 
     ni kutokukata tamaa.
     By Wilma Mankiller.

66.Uzoefu ni Kufanya
     Makosa na kujifunza
     kutokana na Makosa
     hayo.
     By Bill Ackman.

67.Usiogope kuanguka, 
     Bali ogopa sana kubaki
     ulipoangukia.
     By J. Kweka.

68.Kanuni ya Maisha iko
     hivi "Ukitaka kupata
     unachotaka, Saidia
     wengine kupata
     wanachotafuta". 
     By J. Kweka.

69.Ili kufanikiwa tumia
      kanuni hii:-   
Mipango+Pesa+Uwekezaji=Mafanikio.

70.Kama biashara yako
     haina changamoto basi
     mafanikio yake ni
     madogo. 
     By Winston Churchill.

71.Elimu si njia ya
    kuepukana na umaskini,
    Bali ni njia ya
    kupambana na
    Umaskini.By J.K Nyerere.

72.Kabla hujajiona hufai,
     tambua kuna watu
     wakikutazama
     wanajivunia.

73.Ujuzi na maarifa havina
      thamani kama
      havitawekwa kwenye
      matendo.
      By J. Kweka

74.Ukitaka kushinda
     katika mbio kimbia na
     wenzako. Ila ukitaka
     kufika mbali zaidi
     kimbia mwenyewe.

75.Hatukui wakati wa
    utulivu, Bali tunakuwa
    wakati wa changamoto.

76.Wakati wa njaa usiombe
    samaki, Bali  omba ujuzi
    wa kuvua samaki ili
   uweze kula kila siku.

77.Kuna Watu Mafanikio
     Yao Huja Taratibu,
     Lakini Unapomfanyia
     Fitina Unamsaidia
     Kuyafikia Mapema
     Zaidi. By J. Kweka.

78.Ukiona Unashindwa
     Kumdhibiti Adui Yako
     Katika Nia Zake, Basi
     Ungana Naye Kutimiza
     Malengo Yake.

79.Kila Ng'ombe Hujua
    Harufu Ya Mfugaji Wake,
    Hata Mafanikio Huenda
    Kwa Yule Mwenye Kujua
    Kanuni Za Kuyapata,

80.Uwendawazimu
    mmojawapo ni ule wa
    kufanya jambo lile lile 
    kwa staili ile ile huku
    ukitegemea matokeo
    tofauti. 
    By Albert Eistein

81.Ukiona unakosolewa
    kwa kile unachokifanya,
    jua kabisa uko karibu na
    mafanikio. By J. Kweka

82.Hakuna mtu aliyewahi
  kuwa maskini kwa kutoa.
   By Anne Frank

83.Furaha ya maisha yako
     hutegemea ubora wa
     mawazo yako. 
     By Marcus Aurelius

84.Haitoshi tuu kuwa na
    akili nzuri, Bali jinsi
    unavyoweza kuitumia
   vizuri. By Rene Descartes.

85.Tunachojua ni tone,
   Kile ambacho hatujui ni
    bahari. 
   By Sir Isaac Newton

86.Ishi kana kwamba
  utakufa kesho. Jifunze
  kana kwamba ungeishi
  Milele. Mahatma Gandhi.

87.Hekima pekee ya kweli
    ni katika kujua hujui
    chochote. By Socrates

88.Kushindwa ni kitoweo
    kinachokipa mafanikio
    ladha yake. 
    By Truman capote.

89.Fursa huzidisha kadri
     zinavyokamatwa. 
     By Jua Tzu

90.Usihukumu kila siku
   kwa mavuno unayovuna.
   Bali kwa mbegu
   unazopanda. 
   By Robert Louis

91.Hakuna rafiki
   mwaminifu kama kitabu.
   By  Ernest Hemingway

92.Kwa maana ni katika
    kutoa  ndipo tunapokea.
Mtakatifu Francis wa Assisi

93.Sijashindwa, bali
    nimepata tu njia 10,000
    ambazo hazikufanya
    kazi.
    By Thomas Edison

94.Utajiri haumo katika
    kuwa na mali nyingi,
    Bali kwa kuwa na
    mahitaji machache. 
    By Epictetus.

95.Hakuna chochote
   kinachowezekana kwake
   ambaye hatajaribu. 
   By Alexander the Great.

96.Kama hujasimamia
     kwenye kitu chochote,
     Basi chochote chaweza
     kukuangusha. 
     By J. Kweka.

97.Kobe hutembea taratibu
     lakini hajawahi kukosa
     chakula chake.
     By J. Kweka

98.Tembo ni mnyama
     mwenye nguvu nyingi
     lakini huangushwa na
     sisimizi.

99.Tajiri akiugua maskini
     huenda kumsalimia na
     kumpa pole, lakini
     maskini akiugua
     husubiri hadi apone na
    kwenda kwa tajiri  kutoa
     taarifa kuwa alikuwa
     mgonjwa.

100.Masikini hata akitoa
       mawazo mazuri kiasi
       gani kwenye kikao
       ataonekana
       anasumbua, lakini
       tajiri akitukana
       kwenye kikao
       ataonekana anafanya
       utani.


101.Marafiki wakweli
       hupatikana kipindi cha
       shida lakini,
       wanaopatikana kipindi
       cha Mafanikio ni
       wachawi. 
       By  J. Kweka.

102.Nilikuwa najiuliza
       Kwa muda mrefu
       ulemavu wangu ni 
       Upi ndipo nikagundua
     kuwa ni wa kutotambua
       talanta yangu.
       By J. Kweka

103.Kanuni ya mafanikio
  Yako iko hivi:
Effort+Determination
+Prayer =Successful

104.Kwenye wingi wa
    maji ni Mjinga tu ndiye
    anaye weza kuwa na kiu.
    Bob Marley 

105.Mjasiriamali ni yule
      mwenye kuona FURSA
      ambayo wengine
      hawaioni. By J. Kweka

106.Safari ya Maili 1000
      huanza na hatua 1.
      Chinese Proverb

107.Msomi ni yule
      mwemye Uwezo wa
     Kuoanisha kati ya Elimu
      ya Darasani na ile ya
      Mtaani. By J. Kweka

108.Ukiwa na Marafiki 9
       ambao ni Vichaa
      Tambua kabisa wewe ni
      Kichaa wa 10. 
      By J. Kweka

109.Mtu hujichorea ramani
       ya Maisha yake
       mwenyewe, Kwa hiyo
       ichore kwa umakini. 
       By J.Kweka

110.Ukitaka kuishi
       usiogope kufa. Kwa
        maneno mengine,
       Ukitaka kufanikiwa
        katika maisha yako,
        Usiogope Changamoto.
        By J. Kweka

111.Usinionee Huruma,
        Kwani Maisha yangu
        ni kafara ya Mafanikio
        yangu. By J. Kweka

112.Hakuna Ufundi
        mkubwa kama
        Wakuishi na Watu
        Vizuri kwenye hii
        Dunia yenye Sauti
         nyingi. By J. Kweka 

113.Kwenye hii Dunia
       jitahidi sana Hadithi ya
       Maisha yako Isimuliwe
       Vizuri. By J. Kweka

114.Ukiona Mke/Mme wa
       Bosi wako anajifunza
        kuendesha gari ujue
        kuna Ajira ya Mtu iko
        matatani, Kwa hiyo
        kaa tayari kwa kila
        badiliko linalotokea
        kwani Maisha ndivyo
        yalivyo. By J. Kweka

115.Jifunze Kuiona
       Dhahabu hata kama
       ipo kwenye Tope. 
       By J. Kweka

116.Hakiwezi kukamilika
       kitu Chochote kama
       hujakianza. Anza sasa
       bado hujachelewa.
       By J. Kweka

117. Tai ni ndege mwenye
         Uwezo wa kuona
         kitoweo hata akiwa
         mbali, nasi tujifunze
         kuziona FURSA hata
         kama hazionekani.
         By J. Kweka

118.Penye Miti hapana
       Wajenzi, Lakini
       hapakosekani Asali.
       By J. Kweka

119.Ukitaka kupanda juu,
        paheshimu sana pale
        Unapokanyagia. 
        By J. Kweka

120.Kwenye harakati za
       Mafanikio tujifunze
       kutumia neno SISI
       kwani MIMI
       Hakufikishi popote.
       By J. Kweka

121.Mtu Mwenye
       Ushawishi ni wa
       Thamani sana kuliko
       watu 100 Wenye
       Matamanio.
       By Zig Ziglar

122.Ewe Mwanafunzi Soma
       kwa Bidii kwani Tako
       Husinyaa na Kuisha. 
       By Unknown

123.Kinachoshindikana
       kwa Mwenzio kwako
       kinawezekana. Songa
       mbele Usikate Tamaa.
       By J.Kweka

124.Haijalishi mnasema
       nini juu yangu, Bali
       ninachojali ni
       ninapata nini kwenye
       Maisha yangu. Nasonga
       mbele nyuma Mwiko.
       By J. Kweka

125. Ukarimu ndiyo Lugha
         pekee ambayo Kiziwi
         anaweza kuisikia na
         Kipofu anaweza
         Kuiona. 
         By Mark Twain

126.Nilipokuwa mdogo
        niliwatamani sana
        Watu wenye Akili, Kwa
        sasa nimezeeka
        nawatamani Watu
        Wakarimu. 
        By Abraham Heschel

127.Hakuna mtu ambaye
        alishaumizwa Tumbo
        kwa Kumeza Maneno
        Machafu yaliyosemwa
        na Wengine. 
        By Winston Churchill 

128.Tuna Masikio Mawili
        na Mdomo Mmoja ili
        Tusikilize Zaidi kuliko
        Kuongea. By Epictetus

129.Usikubali watu
        Wanaofaidi Wema
        wako Wakufanye
        Uache kuwa Mwema. 
        By J. Kweka

130.Ukarimu wa kweli ni
       ule wa kumsaidia mtu
        kitu ambacho kamwe
        hawezi kukulipa. 
        By Frank A. Clark

131.Ni bora kuwa Upinde
       kwenye Wingu la
       Mwenzako kuliko
       kuwa Ukungu. 
       By Maya Angelou

132.Ulimwengu huu
       umejaa watu wengi
       ambao hawajali
       Chochote; Bali wewe
        kuwa mmojawapo wa
        anayejali sana kwenye
        huu Ulimwengu. 
        By J. Kweka

133.Hakuna aliyewahi
       kupandisha heshima
       yake kwa kushusha ya
       Wengine. By J. Kweka

134.Ulimi wa Kulaumu ni
        Balozi wa Moyo
        Usiokuwa na
        Shukurani.
        By J. Kweka

135.Ukitaka kushinda
       katika biashara yako
       inakubidi ushinde na
       wateja wako.
       By J. Kweka

136.Rafiki mzuri ni yule
        anayekunyanyua
        wakati wengine
        hawaoni kama
        umeanguka.
        By J. Kweka
  


Hamasika na hii Hapa:-
Jack Ma Quotes on Entrepreneurship
Nukuu zaidi za Maisha:-
Mbinu za Kuamsha hamasa ya kufanikiwa kwako:-
Umuhimu wa kuwa na pesa:-

Usikate tamaa bado una nafasi ya kufanikiwa Jackma:-
........................................................................................
Siri 101 za kukuwezesha kuwa na Mafanikio Maishani:-
Ili kufanikiwa Maishani fuata Ushauri huu:-

Siri  13  za Kufahamu kuhusu Pesa:-
Mbinu wanazotumia Matajiri kufanikiwa zaidi:-
Nini cha kufanya ili ufanikiwe katika Maisha?
Mbinu za kukuwezesha kutimiza ndoto zako:-
JackMa ni nani?
Ben Carson ni nani?
Elon Mask ni nani?
Fahamu Chanzo cha utajiri wa Mabilionea hawa:-
Orodha ya Mabilionea wa Kitanzania hii hapa:-

VIDEO ZA KUHAMASISHA:

Misingi 10 ya Fedha na Mafanikio:-
Kanuni za Mafanikio:-

Orodha ya Vitabu Muhimu Kwa Mjasiriamali:-

UCHAMBUZI WA  VITABU MBALIMBALI VITAKAVYO KUINUA KIUCHUMI:-

 Think and Grow Rich:-
Eat that Frog:-

KAMA UMEGUSWA NA UNGEPENDA SAPOTI KAZI YETU HII WAWEZA KUTUMA KIASI CHOCHOTE KWENYE NAMBA HII YA 
M-PESA: 0753775158 - JOACHIM KWEKA
Barikiwa Sana
...............................................................


Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Shakina Pre and Primary English Medium School

Kikatiti Secondary School

Ujasiria mali na Maisha