Nukuu za kutia Moyo Maishani


🖱Hizi ni Nukuu (Quotes) zinazoweza kukuhamasisha Katika kufikia ndoto zako, Binafsi hunipa Ari na Moyo wa Kufanya kazi kwa bidii ili kuyatimiza malengo yangu, natumaini na wewe zinaweza kuwa Kichocheo Kikubwa cha mafanikio kwako pia.


🖱Karibu Tujifunze Pamoja🖱
1.Muujiza uliopo kwenye
kufanikiwa ni kuacha
kutamani na kuanza
kutenda. By J. Kweka

2.Usikubali uoga wako
uamue hatima ya maisha
yako.

3.Anguka mara NANE
lakini simama mara
ya TISA.
Chinese Proveb.

4.Ujasiri siyo Kutokuwepo
kwa HOFU, bali ni
kufanya kitu ingawa
kuna HOFU.

5.Ukitaka kushindwa
kufika unakokwenda ni
kujaribu kumtupia jiwe
kila mbwa anaye
kubwekea njiani.By
Winston Churchhill.

6.Furaha ya Maisha siyo
kuwa na pesa nyingi, bali
ni kuona pesa yako
inasaidia wale
wasiyojiweza.

7.Usipende kufanya
mambo makubwa sana,
Bali fanya yale
madogomadogo kwa
ufanisi mkubwa. By
St. Theresa of Calcutta.

8.Huwezi Kufanikiwa
mpaka upende kazi ile
unayoifanya.
By Dale  Carnegie.

9.Ukitaka kufanya
   mabadiliko makubwa
   katika maisha, acha
   kuangalia ukubwa wa
   tatizo lako. 
   By T. Harv Eker.

10.Watu wengi hawaishi
     ndoto zao, kwa kuwa
     wanaishi uoga wao. 
     By Les Brown

11.Usiache yale usiyoweza
     kufanya yaingilie na
     yale unayoweza
     kufanya.

12.Ni bora kufeli katika
     uhalisia kuliko kufaulu
     katika kuiga. By Herman
     Melville.

13.Vitu vingi vya maana
      katika Dunia vilifanywa
     na watu ambao walizidi
     kujaribu hata pale
     mambo yalivyoonekana
     yameshindikana kabisa.
     Dale Carnegie.

14.Haijawahi kuchorwa
     mahali popote picha ya
     kuvutia ya mtu mvivu.
     By Oprah Winfrey.

15.Mafanikio yako
     hupimwa kwa ukubwa
     wa vikwazo ulivyopitia
     Kufikia Malengo
     yako. By  J.  Kweka.

16.Inakupasa kuamka kila
     asubuhi na hamasa,
     kama unataka kulala
     usiku ukiwa
     umeridhika. By George
     Lorimer.

17.Hamasa ndiyo
     inayokufanya uanze
     safari yako ya
     mafanikio. Tabia ndiyo
     inayokufanya uendelee
     mbele katika mafanikio.
     By Jim Ryun.

18.Uoga wetu katika
     maisha usiwe katika
     kushindwa,  bali katika
     kushinda vitu visivyo na
     maana. By Francis Chan

19.Akili ndogo hushikwa
     na kutishwa na hali
     ngumu,  Wakati Akili
     kubwa huvuka na
     kupanda
     juu ya matatizo.

20.Inaweza ikakubidi
     kupigana katika vita
     zaidi ya mara moja ili
     ushinde.

21.Mafanikio siyo
     kutokufanya makosa,
     Bali ni kuhakikisha
     hurudii kosa ulilolifanya
     zaidi ya mara moja. By
     George Bernard Shaw.

22.Uwekezaji mzuri ni ule
     wa kuwekeza katika
     Maarifa,  kwani
     matunda yake
     utayafaidi daima. 
     By Warren Buffett.

23.Kama unaweza
     kuhesabu hela zako,
     Basi inakubidi ufanye
     kazi kwa bidii sana. 
     By Genius Ginimbi.

24.Kuzaliwa masikini si
     kosa lako,  Bali kufa
     masikini ni kosa lako. 
     By BillGate.

25.Kupata 0 katika
     mtihani haimaanishi
     huwezi, ni kwamba una
     njia nyingine 100 za
     kufanya vizuri zaidi. 
     By J. Kweka.

26.Muda mzuri wa
     kupanda mti ni miaka
     10 iliyopita, lakini muda
     mwingine mzuri zaidi ni
     sasa. Chinese Proverb

27.Kitu pekee
     kinachokutenganisha
     wewe na mafanikio
     yako ni Fikra na
     mtazamo wako.

28.Kuwa hodari kusimamia
     kile unachoamini hata
     kama ukiishia
     kusimama mwenyewe.

29.Ni bora kujaribu na
     kushindwa,  kuliko
     kutojaribu kabisa,
     By Roy T Bennet.

30.Mtu pekee ambaye
     hajawahi kukosea ni 
     yule ambaye hakuwahi 
     kujaribu  kitu kipya.


31.Kuna Wakati utafika
     utagundua muda wa
     kufanya yale Mambo
     Uyapendayo ulishapita,
     Lakini wakati mwingine
     mzuri ni sasa.

32.Hujachelewa kuwa yule
      unayetamani kuwa.

33.Kula chakula kama
     dawa kwa ajili yako;
     Vinginevyo utakuja 
    kula dawa kama chakula
     chako. By Michael Osae

34.Mafanikio ni jumla ya
     nguvu kazi ndogondogo
     zinazorudiwa kila siku.
     By Robert Collier.

35.Mwanzo wa Kila
     Mafanikio ni njaa na kiu
     ya hayo mafanikio. 
     By J. Kweka.

36.Usisubiri fursa itokee,
     Bali Tengeneza fursa
     yako mwenyewe. 
     By Chris Grosser.

37.Wajasiriamali wenye
     mafanikio ni watoaji na
     si wachukuaji.

38.Vitu vizuri huja kwa
      mtu yule anayevisubiri,
      Lakini Mafanikio huja
      kwa mtu mwenye
     kutoka nje na kuyafuata.

39.Kama uko tayari
     kufanya kazi kwa nguvu
     zaidi ya unavyolipwa,
     Mwishowe utalipwa
     zaidi ya kazi
     unayofanya. 
     By J. Kweka.

40.Mafanikio ni
     kinachokuja baada ya
     kuacha kujipa 
     vijisababu.
     By Luis Galarza.

41.Akili yako ina nguvu
      kuliko unavyodhani,  
      Jaza akili yako na
      maneno na fikra
      chanya na utaona
      Mafanikio yake.

42.Ili Ufanikiwe, inakubidi
     Ujaribu kufanya kitu
     kimoja kila siku
     kinachokutisha.

43.Mafanikio 
    yameungwa na
    mipango.     
    Na ukishindwa kupanga,
    Umepanga kushindwa.
    By John Beckley.

44.Ukitaka kuwa wa
     thamani, tengeneza
     thamani kwa wengine
     Kwanza. By J. Kweka.

45.Jifunze Elimu zote,
     Lakini Elimu ya fedha
     ina Umuhimu Wake. 
     By J. Kweka.

46.Katika Maisha Kuna
     siku mbili tu muhimu,
     nazo ni Siku ya
     kuzaliwa na ya pili 
     ni Siku ya Kujua 
     kwanini Ulizaliwa. 
     By J. Kweka.

47.Ukitaka kuwa mtu wa
     mafanikio, Kuwa makini
     sana na kitu Ulacho,
     Usomacho, Uangaliacho
     na Marafiki
     wanaokuzunguka. 
     By J. Kweka.

48.Ukitaka kumla tembo
     usiangalie ukubwa
     wake, Na ukitaka 
     kufanikisha jambo
     Anza kidogokidogo.

49.Vita vya kwanza
    vinavyomtesa binadamu
     ni hofu, na vya pili ni
     kukata tamaa. 
     By J. Kweka

50.Wengi tunatamani
     kusikia kisemwacho,
     lakini hatuna mbinu za
     kusikiliza. By J. Kweka.


51.Usikimbilie Pesa, bali
     penda kile
     unachokifanya na
     kifanye kwa ufanisi
     mkubwa nayo pesa
     itakukimbilia.
     By Samantha Wills.

52.Kufanikiwa ni kama
    fumbo, Ukiona Maisha
    yanakupa Limao; Wewe
    tumia hizo limao
    kutengenezea juisi.
    By J. Kweka.

53.Ukipewa masaa 
     Matano kukata mti, 
     Tumia masaa matatu
     kunolea Shoka.
     By Abraham Lincoln.
    
54.Linda sana mdomo
    wako, Ukiufungua ujue
    Unaiambia dunia kuwa
    wewe ni mtu wa aina
    gani.
    By Les Brown.

55.Tunapata afya kwa kula
     vyakula, na tunapata
     maarifa kwa kusoma
     vitabu. By J. Kweka.

56.Ili kufanikiwa, katika
     kamusi yako futa neno
     "Haiwezekani" 
     By Napoleon Hill.

57.Fursa ni kama embe,
     wakati unasubiri liive,
     wengine wanalila kwa
     chumvi. By J. Kweka.

58.Ukiacha kusoma Vitabu,
      ujue usha anza kufa
      taratibu. By J. Kweka.

59.Usipojiajiri kwenye
     kutimiza ndoto zako,
     Basi utaajiriwa kutimiza
     za mwenzako.

60.Kuwa wa kwanza
     kujaribu na kushindwa, 
     ili upate muda mzuri wa
     kujifunza. By J. Kweka.

61.Kiongozi Bora ni 
     msomaji mzuri wa 
     Vitabu.

62.Silaha nzuri ya
    kutokukosolewa ni hii,
    Usijaribu chochote,
    Usianzishe chochote, na
    Usifanye chochote.
    By J. Kweka.

63.Katika kukamilisha
  safari yako ya mafanikio,  
  Jifunze kukaa kimya. 
  By J. Kweka.

64.Ubunifu ndiyo ajira
     pekee ya Kudumu,
     Kwa hiyo heshimu
     ubunifu wako.
     By J. Kweka

65.Siri ya Mafanikio yetu 
     ni kutokukata tamaa.
     By Wilma Mankiller.

66.Uzoefu ni Kufanya
     Makosa na kujifunza
     kutokana na Makosa
     hayo.
     By Bill Ackman.

67.Usiogope kuanguka, 
     Bali ogopa sana kubaki
     ulipoangukia.
     By J. Kweka.

68.Kanuni ya Maisha iko
     hivi "Ukitaka kupata
     unachotaka, Saidia
     wengine kupata
     wanachotafuta". 
     By J. Kweka.

69.Ili kufanikiwa tumia
      kanuni hii:-   
Mipango+Pesa+Uwekezaji=Mafanikio.

70.Kama biashara yako
     haina changamoto basi
     mafanikio yake ni
     madogo. 
     By Winston Churchill.

71.Elimu si njia ya
    kuepukana na umaskini,
    Bali ni njia ya
    kupambana na
    Umaskini.By J.K Nyerere.

72.Kabla hujajiona hufai,
     tambua kuna watu
     wakikutazama
     wanajivunia.

73.Ujuzi na maarifa havina
      thamani kama
      havitawekwa kwenye
      matendo.
      By J. Kweka

74.Ukitaka kushinda
     katika mbio kimbia na
     wenzako. Ila ukitaka
     kufika mbali zaidi
     kimbia mwenyewe.

75.Hatukui wakati wa
    utulivu, Bali tunakuwa
    wakati wa changamoto.

76.Wakati wa njaa usiombe
    samaki, Bali  omba ujuzi
    wa kuvua samaki ili
   uweze kula kila siku.

77.Kuna Watu Mafanikio
     Yao Huja Taratibu,
     Lakini Unapomfanyia
     Fitina Unamsaidia
     Kuyafikia Mapema
     Zaidi. By J. Kweka.

78.Ukiona Unashindwa
     Kumdhibiti Adui Yako
     Katika Nia Zake, Basi
     Ungana Naye Kutimiza
     Malengo Yake.

79.Kila Ng'ombe Hujua
    Harufu Ya Mfugaji Wake,
    Hata Mafanikio Huenda
    Kwa Yule Mwenye Kujua
    Kanuni Za Kuyapata,

80.Uwendawazimu
    mmojawapo ni ule wa
    kufanya jambo lile lile 
    kwa staili ile ile huku
    ukitegemea matokeo
    tofauti. 
    By Albert Eistein

81.Ukiona unakosolewa
    kwa kile unachokifanya,
    jua kabisa uko karibu na
    mafanikio. By J. Kweka

82.Hakuna mtu aliyewahi
  kuwa maskini kwa kutoa.
   By Anne Frank

83.Furaha ya maisha yako
     hutegemea ubora wa
     mawazo yako. 
     By Marcus Aurelius

84.Haitoshi tuu kuwa na
    akili nzuri, Bali jinsi
    unavyoweza kuitumia
   vizuri. By Rene Descartes.

85.Tunachojua ni tone,
   Kile ambacho hatujui ni
    bahari. 
   By Sir Isaac Newton

86.Ishi kana kwamba
  utakufa kesho. Jifunze
  kana kwamba ungeishi
  Milele. Mahatma Gandhi.

87.Hekima pekee ya kweli
    ni katika kujua hujui
    chochote. By Socrates

88.Kushindwa ni kitoweo
    kinachokipa mafanikio
    ladha yake. 
    By Truman capote.

89.Fursa huzidisha kadri
     zinavyokamatwa. 
     By Jua Tzu

90.Usihukumu kila siku
   kwa mavuno unayovuna.
   Bali kwa mbegu
   unazopanda. 
   By Robert Louis

91.Hakuna rafiki
   mwaminifu kama kitabu.
   By  Ernest Hemingway

92.Kwa maana ni katika
    kutoa  ndipo tunapokea.
Mtakatifu Francis wa Assisi

93.Sijashindwa, bali
    nimepata tu njia 10,000
    ambazo hazikufanya
    kazi.
    By Thomas Edison

94.Utajiri haumo katika
    kuwa na mali nyingi,
    Bali kwa kuwa na
    mahitaji machache. 
    By Epictetus.

95.Hakuna chochote
   kinachowezekana kwake
   ambaye hatajaribu. 
   By Alexander the Great.

96.Kama hujasimamia
     kwenye kitu chochote,
     Basi chochote chaweza
     kukuangusha. 
     By J. Kweka.

97.Kobe hutembea taratibu
     lakini hajawahi kukosa
     chakula chake.
     By J. Kweka

98.Tembo ni mnyama
     mwenye nguvu nyingi
     lakini huangushwa na
     sisimizi.

99.Tajiri akiugua maskini
     huenda kumsalimia na
     kumpa pole, lakini
     maskini akiugua
     husubiri hadi apone na
    kwenda kwa tajiri  kutoa
     taarifa kuwa alikuwa
     mgonjwa.

100.Masikini hata akitoa
       mawazo mazuri kiasi
       gani kwenye kikao
       ataonekana
       anasumbua, lakini
       tajiri akitukana
       kwenye kikao
       ataonekana anafanya
       utani.




101.Marafiki wakweli
       hupatikana kipindi cha
       shida lakini,
       wanaopatikana kipindi
       cha Mafanikio ni
       wachawi. 
       By  J. Kweka.

102.Nilikuwa najiuliza
       Kwa muda mrefu
       ulemavu wangu ni 
       Upi ndipo nikagundua
     kuwa ni wa kutotambua
       talanta yangu.
       By J. Kweka

103.Kanuni ya mafanikio
  Yako iko hivi:
Effort+Determination
+Prayer =Successful

104.Kwenye wingi wa
    maji ni Mjinga tu ndiye
    anaye weza kuwa na kiu.
    Bob Marley 

105.Mjasiriamali ni yule
      mwenye kuona FURSA
      ambayo wengine
      hawaioni. By J. Kweka

106.Safari ya Maili 1000
      huanza na hatua 1.
      Chinese Proverb

107.Msomi ni yule
      mwemye Uwezo wa
     Kuoanisha kati ya Elimu
      ya Darasani na ile ya
      Mtaani. By J. Kweka

108.Ukiwa na Marafiki 9
       ambao ni Vichaa
      Tambua kabisa wewe ni
      Kichaa wa 10. 
      By J. Kweka

109.Mtu hujichorea ramani
       ya Maisha yake
       mwenyewe, Kwa hiyo
       ichore kwa umakini. 
       By J.Kweka

110.Ukitaka kuishi
       usiogope kufa. Kwa
        maneno mengine,
       Ukitaka kufanikiwa
        katika maisha yako,
        Usiogope Changamoto.
        By J. Kweka

111.Usinionee Huruma,
        Kwani Maisha yangu
        ni kafara ya Mafanikio
        yangu. By J. Kweka

112.Hakuna Ufundi
        mkubwa kama
        Wakuishi na Watu
        Vizuri kwenye hii
        Dunia yenye Sauti
         nyingi. By J. Kweka 

113.Kwenye hii Dunia
       jitahidi sana Hadithi ya
       Maisha yako Isimuliwe
       Vizuri. By J. Kweka

114.Ukiona Mke/Mme wa
       Bosi wako anajifunza
        kuendesha gari ujue
        kuna Ajira ya Mtu iko
        matatani, Kwa hiyo
        kaa tayari kwa kila
        badiliko linalotokea
        kwani Maisha ndivyo
        yalivyo. By J. Kweka

115.Jifunze Kuiona
       Dhahabu hata kama
       ipo kwenye Tope. 
       By J. Kweka

116.Hakiwezi kukamilika
       kitu Chochote kama
       hujakianza. Anza sasa
       bado hujachelewa.
       By J. Kweka

117. Tai ni ndege mwenye
         Uwezo wa kuona
         kitoweo hata akiwa
         mbali, nasi tujifunze
         kuziona FURSA hata
         kama hazionekani.
         By J. Kweka

118.Penye Miti hapana
       Wajenzi, Lakini
       hapakosekani Asali.
       By J. Kweka

119.Ukitaka kupanda juu,
        paheshimu sana pale
        Unapokanyagia. 
        By J. Kweka

120.Kwenye harakati za
       Mafanikio tujifunze
       kutumia neno SISI
       kwani MIMI
       Hakufikishi popote.
       By J. Kweka

121.Mtu Mwenye
       Ushawishi ni wa
       Thamani sana kuliko
       watu 100 Wenye
       Matamanio.
       By Zig Ziglar

122.Ewe Mwanafunzi Soma
       kwa Bidii kwani Tako
       Husinyaa na Kuisha. 
       By Unknown

123.Kinachoshindikana
       kwa Mwenzio kwako
       kinawezekana. Songa
       mbele Usikate Tamaa.
       By J.Kweka

124.Haijalishi mnasema
       nini juu yangu, Bali
       ninachojali ni
       ninapata nini kwenye
       Maisha yangu. Nasonga
       mbele nyuma Mwiko.
       By J. Kweka

125. Ukarimu ndiyo Lugha
         pekee ambayo Kiziwi
         anaweza kuisikia na
         Kipofu anaweza
         Kuiona. 
         By Mark Twain

126.Nilipokuwa mdogo
        niliwatamani sana
        Watu wenye Akili, Kwa
        sasa nimezeeka
        nawatamani Watu
        Wakarimu. 
        By Abraham Heschel

127.Hakuna mtu ambaye
        alishaumizwa Tumbo
        kwa Kumeza Maneno
        Machafu yaliyosemwa
        na Wengine. 
        By Winston Churchill 

128.Tuna Masikio Mawili
        na Mdomo Mmoja ili
        Tusikilize Zaidi kuliko
        Kuongea. By Epictetus

129.Usikubali watu
        Wanaofaidi Wema
        wako Wakufanye
        Uache kuwa Mwema. 
        By J. Kweka

130.Ukarimu wa kweli ni
       ule wa kumsaidia mtu
        kitu ambacho kamwe
        hawezi kukulipa. 
        By Frank A. Clark

131.Ni bora kuwa Upinde
       kwenye Wingu la
       Mwenzako kuliko
       kuwa Ukungu. 
       By Maya Angelou

132.Ulimwengu huu
       umejaa watu wengi
       ambao hawajali
       Chochote; Bali wewe
        kuwa mmojawapo wa
        anayejali sana kwenye
        huu Ulimwengu. 
        By J. Kweka

133.Hakuna aliyewahi
       kupandisha heshima
       yake kwa kushusha ya
       Wengine. By J. Kweka

134.Ulimi wa Kulaumu ni
        Balozi wa Moyo
        Usiokuwa na
        Shukurani.
        By J. Kweka

135.Ukitaka kushinda
       katika biashara yako
       inakubidi ushinde na
       wateja wako.
       By J. Kweka

136.Rafiki mzuri ni yule
        anayekunyanyua
        wakati wengine
        hawaoni kama
        umeanguka.
        By J. Kweka

137.Ukiona nimekaa
     Kimya siyo kwamba
     Sina cha kujibu, Bali
     naangalia cha kukujibu
     Kinachoendana na
      Upumbavu wako.

138.Mafundisho ndiyo
     nyenzo pekee 
     inayotumika
     kubadilisha 
    Maisha ya mtu,
    Kwa hiyo kuwa
    makini na
    mafundisho
     Unayopokea kwani
     yanabashiri kesho yako.
     By J.Kweka

139.Siyo kwamba sikuamini,
       Bali siamni marafiki
       wanaokuzunguka.
       By J. Kweka

140.Usiogope Kufa, Bali
    ogopa Kuishi bila Malengo

141.Kujua tu haitoshi
        Ni lazima kuweka
        Katika matendo.
        By J. Kweka

142. Biashara huanza kwa
       wazo dogo lakini hukua
       kwa nidhamu kubwa.

143.Hela hupenda mtu
        anayechukua hatua
        mapema.

144.Mteja mmoja mwenye
    furaha ni mtaji wa biashara
    nyingine nyingi.

145.Usikimbize faida ya
     haraka, jenga biashara ya
     muda mrefu.

146.Biashara si bahati, ni
      maamuzi ya kila siku.

147.Ukiweza kuuza, 
      unaweza kutengeneza
      utajiri wa kudumu.

148.Mtaji mdogo si 
       kikwazo, kukata tamaa
       ndiyo kikwazo.

149.Mafanikio ya biashara
       huanza kwa kuamini
       Kuwa unaweza.

150.Hela huingia kwa mtu
      anayethubutu kuanza.




151.Siri ya biashara ni
     kuwahudumia watu vizuri.

152.Usiogope kuanza kidogo.

153.Mteja akirudi tena, 
      ujue biashara yako ina
      nguvu.

154.Hela huenda pale penye
      ubunifu.

155.Ukijifunza kila siku,
     biashara yako itakua kila
     siku.

156.Wazo moja linaweza
    kubadili maisha yako yote.

157.Tajiri huona fursa
    ambapo wengine wanaona
    shida.

158.Kazi ya biashara ni
     kutatua matatizo ya watu.

159.Faida ni matokeo ya
      huduma nzuri.

160.Biashara ni safari, si
      mbio za siku moja.

161.Ukiwa na nidhamu ya
       fedha, biashara itaishi
       muda mrefu.

162.Hela nyingi huanzia
       kwenye huduma ndogo.

163.Uvumilivu ni mtaji
      mkubwa wa
      mfanyabiashara.

164.Jifunze kuuza kabla
     ya kutafuta mtaji mkubwa.

165.Mjasiriamali wa kweli
       hujifunza kutokana na
       hasara.

166.Biashara inayodumu
      hujengwa na tabia nzuri.

167.Kila siku ni nafasi mpya
      ya kuongeza kipato.

168.Usisubiri mazingira
      mazuri, anza na ulicho
      nacho.

169.Ujasiri huzaa mafanikio
      ya biashara.

170.Biashara ni kujua watu
      wanahitaji nini.

171.Hela hupatikana kwa
      kutoa thamani.

172.Mteja ndiye moyo wa
       biashara yoyote.

173.Ukiwa mwaminifu,
    biashara yako itatangazwa      bure.

174.Mafanikio ya biashara
      hayaji kwa kulalamika.

175.Wafanyabiashara
      wakubwa waliwahi
      kuanza chini kabisa.

176.Kujifunza masoko ni
      kuongeza kipato.

177.Fursa nyingi zipo kwenye
      mahitaji ya kila siku.

178.Hela hupenda mtu
      anayepanga matumizi
      yake.

179.Biashara hukua kwa
      maamuzi sahihi.

180.Mtaji mkubwa bila
     maarifa unaweza kupotea.

181.Ubunifu ni silaha ya
      mfanyabiashara.

182.Kila mteja mpya ni
      mlango wa mafanikio.

183.Usiogope kushindana,
      boresha huduma zako.

184.Biashara nzuri hujulikana
       kwa matokeo yake.

185.Ukiwa na malengo wazi,
      biashara itakuwa rahisi
      kuendesha.

186.Wazo lako lina thamani
      ukilifanyia kazi.

187.Hela haiji kwa kusubiri
       tu.

188.Mafanikio ya biashara
     yanahitaji uvumilivu.

189.Jitahidi kuwa suluhisho
     kwa watu wengi.

190.Biashara ni kujifunza kila
     siku.

191.Faida huongezeka pale
     huduma zinapokuwa bora.

192.Usikate tamaa kwa
  sababu ya mwanzo mgumu.

193.Hela hupatikana kwa
      kufanya kazi kwa akili.

194.Mafanikio huanza na
      nidhamu binafsi.

195.Kila biashara kubwa
     ilianza kama ndoto.

196.Biashara yenye
    mpangilio huleta amani ya
    fedha.

197.Kujituma leo ni utajiri wa
     kesho.

198.Mjasiriamali huona
      nafasi hata kwenye
      changamoto.

199.Kila hatua ndogo inaleta
      maendeleo makubwa.

200.Ukiheshimu wateja,
     biashara itakuheshimu.


201.Hela huenda kwa watu
     wenye uthubutu.

202.Kazi nzuri ni tangazo
     bora la biashara yako.

203.Mafanikio si siri, ni
    juhudi zinazorudiwa.

204.Biashara inahitaji moyo
     wa kujifunza.

205.Kuwa tofauti ndiyo nguvu
     ya biashara.

206.Mteja akiamini bidhaa
     yako, utauza zaidi.

207.Uaminifu hujenga
     biashara inayodumu.

208.Usikubali hofu ikuondoe
      kwenye ndoto zako.

209.Hela hupatikana kwa
      kutatua shida za watu.

210.Biashara ni kuvumilia
       kabla ya kufurahia
       matokeo.

211.Mafanikio ya biashara
      hujengwa taratibu.

212.Usipoteze muda, anza
       sasa.

213.Biashara bora ni ile
      inayowasaidia watu.

214.Ukiwa na malengo
     makubwa, jitihada zako
     zitabadilika.

215.Hela nyingi huja kwa
     nidhamu ndogo ndogo.

216.Kila hasara ina somo
     muhimu.

217.Biashara ni safari ya
      kujiboresha.

218.Usiogope kuanza upya.

219.Hela hupenda watu
     wenye mipango.

220.Biashara ni uhuru
      unaohitaji uwajibikaji.

221.Mafanikio huja kwa 
      watu wanaojaribu tena.

222.Mteja akifurahia huduma
       yako, atawaleta wengine.

223.Biashara nzuri hujengwa
       na maamuzi ya busara.

224.Kila siku ni nafasi ya
      kuongeza mauzo.

225.Ukiwa mbunifu, utaona
      pesa kwenye kila fursa.

226.Biashara inahitaji moyo
      wa kujituma.

227.Mafanikio makubwa
      huanzia hatua ndogo.

228.Hela huja pale thamani
      inapoongezeka.

229.Uvumilivu na nidhamu ni
      msingi wa utajiri.

230.Biashara si kwa watu
    wanaokata tamaa kirahisi.

231.Jifunze kutumia pesa
      kabla ya kutafuta nyingi.

232.Mafanikio huwapenda
      watu wenye uthubutu.

233.Biashara ni njia ya
      kubadili maisha yako.

234.Ukijua mahitaji ya watu,
      hutakosa wateja.

235.Hela ni matokeo ya
      juhudi na maarifa.

236.Ndoto kubwa zinahitaji
      kazi kubwa.

237.Mjasiriamali wa kweli
   haachi kuamini kesho bora.

238.Biashara nzuri
  hujengwa na uaminifu

239.Kila tatizo linaweza
     kuwa chanzo cha
     biashara.

240.Fursa zipo kila
     mahali kwa macho
     yanayoona.

241.Mjasiriamali
      hujifunza zaidi
      kuliko kulalamika.

242.If you don't take any risk
      In life.., In life any Risk will
      Take you.
      By J. Kweka.





Change your Mindset and Your Life will Change too:-

Hamasika na hii Hapa:-
Jack Ma Quotes on Entrepreneurship
Richmindset Vs Poor Mindset Inspired by Jackma
Siri ya Kufanikiwa ni kuanza Kuishi Future yako leo:-
Mbinu za Kuamsha hamasa ya kufanikiwa kwako:-
Utajiri wako uko kwenye Akili yako, Sikiliza hii:-
Vitu Muhimu Vitano(5)
Vya kujifunza kutoka kwa Waliofanikiwa
Umuhimu wa kuwa na pesa:-




Usikate tamaa bado una nafasi ya kufanikiwa Jackma:-
.......................................................
Siri 101 za kukuwezesha kuwa na Mafanikio Maishani:-
Ili kufanikiwa Maishani fuata Ushauri huu:-

Siri  13  za Kufahamu kuhusu Pesa:-
Mbinu wanazotumia Matajiri kufanikiwa zaidi:-
Nini cha kufanya ili ufanikiwe katika Maisha?
Mbinu za kukuwezesha kutimiza ndoto zako:-

Mbinu za kukuwezesha kupata mtaji wa kuanzisha Biashara ya ndoto zako:-

Mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kuanzisha Kampuni au Biashara:-


JackMa ni nani?
Bill gate ni nani?

Fahamu Chanzo cha utajiri wa Mabilionea hawa:-

VIDEO ZA KUKUHAMASISHA:

Misingi 10 ya Fedha na Mafanikio:-
Kanuni za Mafanikio:-

Orodha ya Vitabu Muhimu Kwa Mjasiriamali:-

The Magic of Thinking Big:-

UCHAMBUZI WA  VITABU MBALIMBALI VITAKAVYO KUINUA KIUCHUMI:-

 Think and Grow Rich:-

KAMA UMEGUSWA NA UNGEPENDA SAPOTI KAZI YETU HII WAWEZA KUTUMA KIASI CHOCHOTE KWENYE NAMBA HII YA 
M-PESA: 0753775158 - JOACHIM KWEKA
Barikiwa Sana
.................................................................







Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

The Best Learning Hub in Tz

EntrePreneurship Learning Centre