Nidhamu ya Pesa
Vitu vya Kuzingatia ili kuwa na nidhamu ya pesa:
Mambo 12 katika pesa ambayo unapaswa kuzingatia ni haya:-
1. Usikope pesa ya riba ili
uanzishe biashara.
Usitegemee pesa ya mkopo
kuianzishia biashara, upate
faida kisha uirudishe pesa ya
mkopo na riba yake.
2. Usitumie pesa ambayo bado
haipo mikononi mwako.
Wala usije ukamuahidi mtu
kumpa pesa ambayo
umeahidiwa mahali fulani.
Kama kuna mtu kakwambia,
Flan njoo kesho nikulipe deni
lako - Basi wewe usiende
kukopa vitu dukani au
kumuahidi mtu mwingine
kumpa pesa ambayo
na wewe umeahidiwa.
3. Kama unataka
kuhifadhi/kutunza pesa, kila
unapopata pesa usianze
kuitumia kwanza kisha
ukategemea kutunza kiasi
kitakachosalia.
Hivyo basi, ukipata tu pesa,
weka pembeni kiasi
unachodhani kinafaa
kutunzwa/kuhifadhiwa
kisha tumia kiasi kilichobaki.
4. Ukipata nafasi ya kuonana
na mtu tajiri, kamwe
usiombe pesa.
Bali Omba maarifa ya
kutengeneza pesa kama yeye,
tena kwa mtaji mdogo.
Maarifa ndio mtaji wa kwanza.
Unaweza kupewa/kusaidiwa
Unaweza kupewa/kusaidiwa
pesa iwapo una mawazo
mazuri ya kuzalisha pesa.
Baadhi husema,
"Omba ndoano, usiombe samaki"
5.Usitunze mbegu badala ya
kuipanda. Watu wengi
hufurahia pesa wanayolipwa
/kuipata kisha wanaiweka
benki au nyumbani bila
kuiwekeza. Wekeza pesa
ili uzalishe zaidi. Usiogope
kuingia hasara, kila
aliefanikiwa alipoteza
kwanza kabla hajafanikiwa.
Wengi walipoteza muda,
pesa, afya na hata matumaini
ya kufanikiwa, ila kwa
uthubutu wao, mwisho wa
Siku walifanikiwa”
6.Kamwe usimkopeshe mtu
pesa ambayo unahisi
hatorudisha. Unapomkopesha
mtu huyo pesa, jiridhishe
mwenyewe moyoni kuwa
kama hatoweza kulipa basi
deni lake-halitoathiri urafiki
wenu. Ukihisi kwamba
kushindwa kwake kulipa
kunaweza kuathiri urafiki
wenu, basi mshauri aende
benki akakope”
7. Usikubali kumdamini mtu
ambae huna uhakika kuwa
atalipa kile unachomdhamini.
Kumbuka- dhamana maana
Kumbuka- dhamana maana
yake utawajibika iwapo
atashindwa kulipa.
8. Epuka kutembea na pesa
nyingi ambazo hata huna
matumizi nazo wakati huo.
Unaweza kujikuta unafanya
matumizi ambayo hayakuwa
kwenye ratiba sababu ya
ushawishi wa pesa ya mfukoni.
Ili kuepuka haya, tembea na
Ili kuepuka haya, tembea na
pesa uliyopanga kuitumia
katika safari yako.
Pesa nyingine itunze
Pesa nyingine itunze
mahali pengine palipo
salama”
9. Epuka kutunza pesa mahali
pasipo sahihi. Maeneo kama
kwenye soksi, sidiria, chini
ya mto wa kulalia, chini ya
begi, kwenye kopo au hata
kwenye begi la safari,
si maeneo salama.
~Ni rahisi kusahau, kuibiwa
~Ni rahisi kusahau, kuibiwa
au kupoteza pesa zako.
Ni bora ukatunza pesa
kielektroniki; yaani benki au
kwenye simu au kwenye pochi
yenye kamba ngumu ya kuivaa
mabegani au wallet ambayo
inatosha kwenye mifuko imara
na yenye vifungo kwenye nguo
zako hasa uwapo safarini.
10. Usitumie pesa kwa kitu
ambacho hakikuwa kwenye
ratiba yako.
Jiulize kwanza kabla hujanunua,
"Bila kitu hiki, maisha
yataenda au lah?” Ukiona
maisha yataenda bila kitu
hicho, acha kukinunua.
Tabasamu kisha ondoka.
11. Matumizi yako ya pesa
yasizidi pato lako.
Unaweza kuwa una ndoto
kubwa/matumizi makubwa
ya pesa kuzidi pato lako.
Unapaswa kuwa bahili
katika matumizi yako.
Cheza na pato lako.
Fanya matumizi
makubwa pale tu pato lako
litakapoongezeka. Hii
itakuepushia kushindwa
kufanya baadhi ya mambo
ya msingi na kisha ukajikuta
unaishia kwenye madeni
makubwa.
12. Una ndoto kubwa hapo
baadae; labda kujenga
nyumba, kununua gari,
kununua kiwanja, simu
nzuri hata pikipiki.
Usikurupuke, ukanunua
kitu cha ndoto yako sasa
eti tu sababu umekipata
kwa bei ya punguzo.
Usichanganye kati ya mahitaji
ya baadae na ya sasa.
Pesa unayotumia kutimizia
ndoto sasa itumie kwa mahitaji
ya sasa. Ndoto ibaki kuwa
ndoto. Hii itakuepushia
kuingia katika madeni au
kuishi kwa shida sababu ya
tamaa. Jipange taratibu
kutimiza ndoto yako.
Mkopo ni nini?
Siri za kufahamu juu ya fedha:-
Ufahamu zaidi juu ya Fedha:-
Amri Tano za kupata fedha
Part One:-
Amri tano za kupata Fedha
Part two:-
Kanuni 12 za kupata pesa:-
Tujifunze kutoka kwa Warren Buffet namna ya kupata pesa:-
Tatizo la wengi si ukosefu wa pesa, bali ni namna ya kuitawala pesa:-
Namna ya kutunza hela:-
Nunua Assert na si Liability:-
Mambo usiyoyajua kuhusu Pesa:-
Sababu za kushika hela na kuishia kuwa maskini:-
Umuhimu wa kuwa na hela:-
Matumizi sahihi ya Pesa:-
Muone Dada aliyeacha kazi na kuwa Milionea:-
Mbinu za Kupanga Bajeti na kuweza kuwekeza kwa Haraka zaidi:-
Misingi 10 ya Fedha na Mafanikio:-
Sheria juu ya Uchezeaji wa Fedha nchini Tanzania:-
............................................................................
Asante mwalimu
JibuFuta